Page 10 - SWAHILI_SB01Creation
P. 10
Siku ya tano ya juma la uumbaji, Mungu
aliijaza bahati na viumbe vinavyoishi.
Mungu akasema, Maji na yajawe kwa wingi
na viumbe vyenye vyenye uhai, na ndege
wapae katika anga la mbingu.
Basi Mungu akaumba nyangumi
viumbe wakubwa wa baharini, na kila
kiumbe chenye uhai kiendacho majini,
ambavyo vilijaa baharini kwa wingi wa
jinsi zao, na kila ndege arukaye,
sawasawa na jinsi yake.
Na Mungu akaona ya kuwa
ni vyema.
Mungu akavibarikia, akisema, "Zaeni,
mkaongezeke, mkayajaze maji ya baharini,
ndege na wazidi katika nchi.
Ikawa jioni na baadaye asubuhi,
siku ya tano.
Mwanzo 1:20-23