Page 8 - SWAHILI_SB01Creation
P. 8
Katika siku ya nne ya juma la uumbaji, Mungu aliumba
jua, mwezi na nyota, mbingu pana.
Mungu akasema, Na iwe mianga katika anga la mbingu ili
itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili ya majira
na siku na miaka; tena iwe ndiyo mianga katika anga la
mbingu itie nuru juu ya nchi.
Na ikawa hivyo. Mungu akafanya mianga miwili
mikubwa, ule mkubwa utawale mchana, na ule mdogo
utawale usiku; akafanya na nyota pia.
Mungu akaiweka katika anga la mbingu ili itie nuru
juu ya nchi, kutawala mchana na usiku na kuitenga
Kati ya nuru na Giza
Na Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
Ikawa jioni na baadaye asubuhi, siku ya nne.
Mwanzo 1:14-19