Page 7 - SWAHILI_SB01Creation
P. 7
Mungu akasema, "Maji yaliyo chini ya mbingu
na yakusanyike mahali pamoja, udongo
mkavu uonekane."
Ikawa hivyo. Mungu akauita ule udongo
mkavu, Nchi; na makusanyiko ya maji
akayaita Bahari.
Na Mungu akaona ya
kuwa ni vyema.
Mungu akasema, "Nchi na itoe majani, miche itoayo
mbegu, na miti ya matunda izaayo matunda kwa jinsi
yake, ambayo mbegu zake zimo ndani yake, juu ya
nchi," ikawa hivyo.
Nchi ikatoa majani, miche itoayo mbegu kwa
jinsi yake, na miti izaayo matunda, ambao
mbegu zake zimo ndani yake, kwa jinsi yake.
Mungu akaona ya kuwa
ni vyema.
Ikawa jioni na baadaye asubuhi,
siku ya tatu.
Mwanzo 1:9-13